MTANGAZAJI wa kituo cha
chanel ten Bond Bin Slim ambaeye inadaiwa hivi sasa ni yuko katika
mahusiano na mjane wa aliyekuwa staa wa filamu Bongo marehemu Said Juma
Kilowoko "Sajuki", Wastara Juma amesema siku chache kabla ya mnyange
Jack Cliff hajaelekea China ambako alidakwa na dawa za kulevya,
alimtolea maneno machafu na dharau na kukataa kupokea kitita cha milioni
2 za kitanzania kama malipo ya kufanya filamu pamoja na Wastara.
Bond alisema kwamba alimpigia simu Jack na kumueleza Ishu hiyo kwani alikuwa miongoni mwa wasanii walioonekana kufaa kucheza filamu lakini mwanadada huyo alimsonya kwa dharau na kumtakia manno machafu na mazito huku akisema hana shida na visenti kama milioni mbili. "Siongei kwasababu Jack amekamatwa huo ndiyo ukweli.alikataa katakata kupokea pesa hizo na kudai kwamba ni vijihela kwake ambavyo haviangaikii kwa kucheza filamu. Alisema eti mi nimeona hela milioni mbili??" Alifunguka Bond

"Milioni mbili ni pesa nyingi sana kumlipa msanii wa kike hapa Tanzania ili acheze filamu tena vipande vichache. Wasanii wanalilia nafasi hiyo. Nilisikitika sana kwa mtu kama Jack ambaye hana jina kubwa kwenye filamu kukataa tena kwa maneno ya dharau.
"Kukamatwa kwake huko kumenipa picha fulani. Dada zetu wengi wana matatizo sana unapowahitaji kwenye filamu kwasababu wanadai wana pesa nyingi. Hivi kupokea milioni mbili yangu na kubebeshwa mzigo kisha kukamatwa kipi bora??. Alimaliza kwa kusema hayo Bond
0 comments:
Post a Comment